Friday, May 9, 2025
Home Makala Fadlu Ahitajika Morocco

Fadlu Ahitajika Morocco

by Sports Leo
0 comments

Kwa mujibu wa ripoti kutoka nchini Morocco zinaeleza kuwa klabu ya FAR Rabat ya nchini humo imetuma ofa kwenda klabu ya Simba kwaajili ya kuihitaji saini ya kocha wa klabu ya Simba Fadlu Davies.

FAR Rabat imemtimua kocha wake Hubert Velud na wanahitaji kocha mwingine ambaye ataiongoza klabu hiyo kufikia malengo yao na Fadlu ndiye lengo lao kubwa kwa sasa.

Hata hivyo klabu hiyo itakua na kazi kubwa ya kufanya ili kumnasa kocha huyo kutokana  na kuwa na mkataba na klabu hiyo aliyojiunga nayo msimu huu.

banner

Pia pamoja na hilo FAR Rabat watapata wakati mgumu kutokana na kocha huyo kuwa na project ndefu na klabu hiyo ya kuirudisha katika makali yake baada ya kukosa ubingwa kwa takribani misimu mitatu.

Fadlu amefanikiwa kuirudisha Simba Sc katika makali yake ambapo kwanza imekua na soka la kuvutia huku ikipata alama katika michezo ya ndani na nje ya nchi kiasi cha kufanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.