Wednesday, May 7, 2025
Home Soka Xavi Akubali Yaishe Barcelona

Xavi Akubali Yaishe Barcelona

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa timu ya Barcelona Xavi Hernandez amekubali kuachia ngazi kuifundisha timu hiyo mwishoni mwa msimu huu hasa baada ya kukubali kipigo cha mabao 5-3 kutoka kwa Villareal katika michuano ya ligi kuu nchini humo.

Kocha huyo ambaye alikua staa wa zamani wa kikosi cha Barcelona alipewa nafasi ya kuinoa timu hiyo kukiwa na matarajio makubwa kuwa atafanya vizuri lakini imekua kinyume na matarajio ya wengi baada ya kuwa na mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha klabuni humo.

Kipigo hicho kimeifanya Barca kubaki nyuma kwa alama 10 dhidi ya vinara wa Ligi Real Madrid ambao mapema leo wameendeleza moto kwa ushindi wa mabao 2-1 ugenini dhidi ya Las Palmas.

banner

Mara baada ya kipigo hicho cha Barca Xavi ameonekana kuwa na uso wa simanzi nzito akitafakari kabla ya kwenda kutangaza uamuzi huo mgumu ambao ulitarajiwa na wengi.

Msimu huu Barca chini ya Xavi kwenye mechi zake 21 za Ligi imefanikiwa kushinda 13 ikipoteza 3 na kutoa sare 5, ikiwa nafasi ya tatu na alama zao 44 huku Girona wakiwa nafasi ya pili na alama zao 52.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.