Connect with us

Soka

“Siogopi Kufukuzwa”-Zahera

Kocha wa klabu ya Yanga Mwinyi Zahera amesema haogopi kufukuzwa katika klabu hiyo nan yupo tayari kuondoka endapo uongozi utasitisha mkataba wake unaoisha mwishoni mwa mwaka huu.

Zahera amekua na wakati mgumu klabuni hapo kufuatia matokea mabaya inayopata timu hiyo hasa baada ya kufungwa na Pyramids Fc katika mchezo wa kimataifa iliofanyika jijini Mwanza na kupelekea mashabiki kumrushia chupa za maji.

“Mashabiki ni kawaida yao kuwa wakali siku zote wanataka kuona timu inashinda siku zote kwahiyo sikushanga ile hali”.Alisema Zahera.

Tetesi za kutimuliwa kwa kocha huyo zimezidi kusambaa huku makocha wa zamani waliowahi kuinoa klabu hiyo kama Hans van de pluijm na Erne Brandts wakihusishwa kurejea klabuni hapo pamoja na kocha msaidizi wa klabu ya As vita Raul Shungu na kocha wa zamani wa taifa stars Kim Poulsen.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka