Connect with us

Soka

Kocha Yanga Kutua Kesho

Kocha Mkuu wa Yanga, Luc Eymael atawasili kesho Jumatano saa 7:20 mchana tayari kuungana na kikosi kwa ajili ya mwendelezo wa mechi za Ligi na Kombe la FA akitokea nchini Ubeligiji alikokua mapumzikoni baada ya ligi kusimamishwa kufuatia kusambaa kwa maambukizi ya Virusi vya Corona nchini.

Luc anatarajiwa kuwasili kesho saa saba mchana baada ya kuchelewa kupata ndege kufuatia nchi nyingi duniani kufunga mipaka na anga la ndege.

Taarifa za kocha huyo kuwasili nchini zimethibitishwa na klabu ya Yanga kupitia mtandao wa Yanga App ambako mpaka sasa zaidi wananchama 26000 wamejiunga kupata habari za klabu hiyo.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka