Thursday, May 15, 2025
Home Soka Chelsea Macho Yote Kwa Kai Havertz

Chelsea Macho Yote Kwa Kai Havertz

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa Chelsea  Frank Lampard amewahimiza mabosi kuwa anataka kuinasa saini ya kiungo mshambuliaji Hai Havertz kutoka Bayern Leverkusen katika dirisha lijalo la usajili la  majira ya joto.

Leverkusen hawajapokea ofa rasmi kwa ajili nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 lakini inaaminika Real Madrid pamoja na Bayern Munchen wameshafanya mazungumzo na klabu hiyo huku awali ilidaiwa kuwa Chelsea ipo mbioni kumsaini lakini inaonekana bado dili bichi.

Mpaka sasa Havertz  ameshafunga magoli 11 na Assist 5 katika mechi 26 za Ligi Kuu ya Ujerumani msimu huu huku mkataba wake na Leverkusen ukifikia tamati 30 Juni, 2022.

banner

Inasemekana bosi wa Chelsea Roman Abramovich yuko tayari kutoa kiasi kikubwa cha pesa kumsajili kinda huyo baada ya kukubaliana na klabu ya Rb Leipzig juu ya mshambuliaji Timo Werner.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.