Tuesday, May 6, 2025
Home Makala Meddie Kagere Awalaza Chali Namungo Fc

Meddie Kagere Awalaza Chali Namungo Fc

by Sports Leo
0 comments

Simba Sc jana ilikuwa  ikicheza na Namungo Fc uwanja wa taifa katika mechi ya michuano ya ligi kuu inayoendelea ambapo Simba wameibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Namungo Fc.

Bao la kwanza Simba lilipatikana dakika ya 21 kupitia Francis Kahata ambalo lilisawazishwa na Bigirimana Blaise dakika ya 35 kutokea Namungo Fc huku Simba kabla ya kwenda mapumziko waliongeza bao la pili dakika ya 38 kupitia Hassan Dilunga.

Namungo walijipatia bao la pili dakika ya 70 kupitia Lusajo ambaye aliachia shuti kali akiwa nje ya 18 na kumfanya Kakolanya kuambulia kuokota mpira nyavuni.

banner

Meddie Kagere ambaye ni mshambuliaji   wa Simba aliwachapa Namungo bao la tatu dakika ya 88 na kuwafanya walale chali kwani alimaliza shughuli uwanjani kwa kufunga bao la ushindi ambalo limewapa timu yake pointi 3.

Simba inafikisha jumla ya pointi 44 ikiwa nafasi ya kwanza na imefunga jumla ya mabao 38.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.