Tuesday, May 6, 2025
Home Makala Kichuya Na Wengine Sita Kuikosa Fainali FA

Kichuya Na Wengine Sita Kuikosa Fainali FA

by Sports Leo
0 comments

Simba Sc inatarajiwa kucheza fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Namungo fc siku ya Jumapili Agosti 2, Uwanja wa Nelson Mandela

Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote kupambania taji hilo muhimu kwani timu itakayo shinda na kunyakua kombe ndiyo itakayo iwakilisha nchi kwenye michuano ya kimataifa kwenye Kombe la Shirikisho.

Patrick Rweyemamu amabaye ni meneja wa Simba amesema kuwa kikosi ambacho kilikwenda Tanga kucheza na Coastal Union kisha kikamalizana na Polisi Tanzania kule Moshi ndicho ambacho kitaelekea Sumbawanga.

banner

Wachezaji ambao walikosa michezo hiyo miwili na inatarajiwa watakosa fainali ni Ibrahim Ajib, Sharaf Shiboub, Rashid Juma, Haruna Shamte, Shiza Kichuya, Cyprian Kipenye na Tairone Santos.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.