Connect with us

Soka

Yanga,Prisons Hapatoshi Taifa

Jumamosi kikosi cha Yanga kitashuka kwenye uwanja wa Taifa kuikabili Tanzania Prisons kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom

Mchezo huo utapigwa saa moja jioni

Bila shaka itakuwa siku nyingine kwa kiungo mshambuliaji Bernard Morrisons kuwaongoza mabingwa hao wa kihistoria kusaka ushindi muhimu

Tangu asajiliwe na Yanga mwezi uliopita, Morrison amekuwa na kiwango bora akifunga mabao mawili na kutoa pasi tatu za mabao

Ni mchezo ambao Yanga itahitaji matokeo ya ushindi hasa baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Mbeya City kwenye mchezo uliopita

Afisa Mhamasishaji wa Yanga Antonio Nugaz amethibitisha kuwa mchezo huo utapigwa uwanja wa Taifa ambapo ametaja viingilio kuwa VIP A ni Tsh15,000/-. VIP B na C ni Tsh10,000/- na Mzunguuko ni Tsh5,000/-

Hii itakuwa mara ya pili kwa Morrison kuikabili Tanzania Prisons msimu huu, alikuwemo kwenye kikosi kilichoikabili timu hiyo mchezo wa kombe la FA (ASFC)

Ni katika mchezo huo ambalo alifanya tukio la kutembea juu ya mpira ambalo video yake ilisambaa sana kwenye mitandao ya kijamii

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka