Friday, May 9, 2025
Home Soka Simba yataja Afisa habari mpya

Simba yataja Afisa habari mpya

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Simba imemtangaza mtangazaji wa michezo wa Azam media Ahmed Ally kuwa Afisa habari na mawasiliano mpya wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Ezekiel Kamwaga aliyekuwa akikaimu baada ya kuondoka kwa Haji Manara.

Mwanahabari huyo mwenye uzoefu wa kutosha katika tasnia hiyo,amefanya kazi kwa muda mrefu kwenye vituo vya Sahara media kupitia startv kabla ya kuelekea Azam tv baada ya kujizolea umaarufu mkubwa kwa wadau wa michezo mbalimbali hapa Tanzania.

Ahmed ameshafanya kazi na Simba katika matukio na hafla mbalimbali za klabu hiyo kama vile hafla za utoaji wa tuzo kwa wachezaji waliofanya vizuri,na anajulikana kwa jinsi anavyoipamba timu hiyo kila anapokuwa kwenye majukumu yake ya kikazi katika kituo chake cha Azam tv.

banner

Hata hivyo wadau mbalimbali wa soka nchini wanasubiri kuona ni kitu gani ataenda kuifanyia klabu hiyo kutokana na kazi nzuri iliyofanywa na watangulizi wake kipindi cha nyuma,lakini hakuna shaka juu ya taaluma wake na uwezo wa kushughulika na maswala ya aina hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.