Connect with us

Soka

Molinga,Luc Wawafata Mwadui Kibabe

Kocha wa klabu ya Yanga Luc Eymael pamoja na mshambuliaji David Molinga wamepanda ndege kuelekea mjini Shinyanga kuwavaa Mwadui Fc kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania bara utakaofanyika hapo kesho.

Awali Luc alichelewa kuwasili baada ya kukosa ndege kuja nchini hivyo kuikuta timu ikiwa imetangulia kwa basi wakati Molinga aliachwa baada ya kutokea sintofahamu huku ikielezwa kuwa ana matatizo ya kinidhamu japo mwenyewe alikanusha habari hizo.

Kusafiri kwa wawili hao ni nafuu kwa mashabiki wa Yanga sc kuelekea mchezo huo baada ya timu hiyo kukosa utulivu hasa katika uongozi kutokana na migongano kadhaa inayojitokeza.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka