Connect with us

Soka

Molinga Azua Sekeseke Yanga

Mshambuliaji wa klabu ya Yanga David Molinga amegoma kusafiri na timu kwenda mkoani Shinyanga kucheza na Mwadui kwa kudai kuwa timu hiyo inapendelea baadhi ya wachezaji.

Molinga amelalamika kwa madai ya kuwa kocha Bonifasi Mkwasa anawapendelea baadhi ya mastaa katika timu hiyo wakiwemo Haruna Niyonzima na Benard Morrison kwa madai ya kuwapa nafasi mara kwa mara hata kama hawajafanya mazoezi na timu.

Staa huyo aliyebakiza mkataba wa miaka miwili katika klabu hiyo amedai kwamba mkataba wake utakapoisha ataondoka klabuni hapo kwa kuwa anaona hahitajiki.

Yanga imesafiri leo kuwafata Mwadui Fc mkoani Shinyanga kwa kutumia usafiri wa basi huku ikiacha baadhi ya mastaa kwa sababu mbalimbali.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka