Home Soka Man Utd Yapiga 4

Man Utd Yapiga 4

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Manchester United imeibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Istanbul BasakSeher ya nchini Uturuki katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya usiku wa kuamkia leo.

Bruno Fernandes alifunga mara mbili dakika za 7 na 19 na kuweka rekodi ya kuhusika katika mabao 34 katika mechi 35 alizoichezea Man United tangu ajiunge nao akifunga mara 21 na kusaidia upatikanaji wa mabao 13.

Marcus Rashford alifunga kwa penati dakika ya 34 huku Daniel James akifunga pia dakika ya mwishoni na kuifanya United kufikisha alama 9 katika msimamo wa kundi H wakihitaji alama moja kufuzu hatua ya 16 bora.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited