Wednesday, May 7, 2025
Home Soka Leicester yaipunguza kasi Liverpool

Leicester yaipunguza kasi Liverpool

by Sports Leo
0 comments

Leicester city wameizuia Liverpool kuendelea kuwabana kileleni vinara Manchester city baada ya usiku wa kuamkia leo kuwapa kipigo cha 1-0 kwenye mchezo wa ligi kuu soka nchini Uingereza.

Bao pekee la mchezo liliwekwa kimiani na winga hatari Ademola Lookman kunako dakika ya 59 baada ya kumalizia kazi nzuri ya kiung Dewsburry Hall.

Liverpool wangeweza kupata bao la uongozi kipindi cha kwanza baada ya kupata penati,hata hivyo mshambuliaji Mohamed Salah alikosa mkwaju huyo ukiokolewa na golikipa Kasper Schmeichel na licha ya mpira kurudi kwa Salah lakini bado pia alishindwa kuweka kimiani.

banner

Kwa matokeo hayo sasa Manchester city wanaendelea kjikita kileleni kwa tofauti ya pointi sita nyuma ya Liverpool na Chelsea waliofungana alama,huku city wao wakishuka dimbani Jumatano hii kucheza dhidi ya Brentford.

Matokeo mengine ya ligi hiyo kwa mechi za jana: Southampton 1-1 Tottenham, Watford 1-4 West Ham,Crystal Palace 3-0 Norwich.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.