Thursday, May 8, 2025
Home Makala Azam Fc Wazindua Rasmi Jezi za 2024/2025

Azam Fc Wazindua Rasmi Jezi za 2024/2025

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imezindua rasmi jezi zake za msimu ujao wa ligi kuu na michuano ya kimataifa mapema hii leo katika boti ya Azam Marine wakielekea Visiwani Zanzibar huku wakishuhudiwa na maelfu ya mashabiki kupitia Azam Tv.

Jezi hizo za aina tatu za nyumbani,Ugenini na jezi ya tatu zimezinduliwa mchana wa leo zikiwa na rangi nyeupe,Blue na Nyeusi huku zote zikiwa zimechanganywa na rangi ya dhahabu mbele ya Mh.Tabia Mwita ambaye ni Waziri wa michezo Visiwani Zanzibar.

banner

Mpaka sasa tayari jezi hizo zinapatikana katika maduka mbalimbali Zanzibar na ndani ya jiji la Dar es salaam.

Msimu huu Azam Fc sambamba na kumaliza wa pili katika ligi kuu nchini pia watashiriki michuano ya kimataifa baada ya kupata nafasi ya kushiriki michuano ya klabu bingwa barani Afrika na wanatarajiwa kuanza na Apr ya Rwanda katika hatua ya awali.

 

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.