Home Soka Azam Fc Wazindua Rasmi Jezi za 2024/2025

Azam Fc Wazindua Rasmi Jezi za 2024/2025

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imezindua rasmi jezi zake za msimu ujao wa ligi kuu na michuano ya kimataifa mapema hii leo katika boti ya Azam Marine wakielekea Visiwani Zanzibar huku wakishuhudiwa na maelfu ya mashabiki kupitia Azam Tv.

Jezi hizo za aina tatu za nyumbani,Ugenini na jezi ya tatu zimezinduliwa mchana wa leo zikiwa na rangi nyeupe,Blue na Nyeusi huku zote zikiwa zimechanganywa na rangi ya dhahabu mbele ya Mh.Tabia Mwita ambaye ni Waziri wa michezo Visiwani Zanzibar.

banner

Mpaka sasa tayari jezi hizo zinapatikana katika maduka mbalimbali Zanzibar na ndani ya jiji la Dar es salaam.

Msimu huu Azam Fc sambamba na kumaliza wa pili katika ligi kuu nchini pia watashiriki michuano ya kimataifa baada ya kupata nafasi ya kushiriki michuano ya klabu bingwa barani Afrika na wanatarajiwa kuanza na Apr ya Rwanda katika hatua ya awali.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited