by Sports Leo
0 comments

Bondia Mtanzania Fadhili Majiha ‘Kiepe Nyani’ ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC Afrika ameweka rekodi ya kuwa Bondia wa kwanza nchini kupata hadhi ya nyota nne na nusu akivunja rekodi ya  mabondia Hassan Mwanyiko na Tony Rashid katika Mtandao wa maalumu wa Takwimu za mabondia wa Boxrec.

Bondia huyo amefikia kiwango hicho wiki moja baada ya kushinda kwa pointi dhidi ya mpinzani wake  Bongani Mahlangu wa Afrika Kusini katika pambano la Raundi 10 lililoffanyika katika ukumbu wa sabasaba wilayani Temeke.

Pamoja na kufikisha hadhi hiyo Pia ameingia kwenye orodha ya Mabondia 10 Bora Duniani uzani wa Bantam, akishika nafasi ya 7 kati ya 1,056.

banner

Mwakinyo ndiye Bondia wa kwanza Nchini kufikia Hadhi ya Nyota 4 lakini kwa sasa ameshuka mpaka nyota 2 katika uzani wa Super Walter wakati Tony Rashid ana Nyota 2.5 katika Uzani wa Super Bantam.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited