Friday, May 9, 2025
Home Makala Yanga Kumlipia Morrison Cas

Yanga Kumlipia Morrison Cas

by Sports Leo
0 comments

Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela amekiri timu hiyo kudaiwa na wanaendelea kulipa madeni hayo ambayo mengi wameyarithi kutoka katika uongozi uliopita.

Jana kuliibuka taarifa kuwa Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhisi wa Michezo (CAS) imeiamuru klabu ya Yanga kumlipa dola 20,000 aliyekuwa mshambuliaji wake Amissi Tambwe ikiwa ni madai ya fedha za usajili na malimbikizo ya mishahara ya miezi mitatu

Mwakalebela amesema uongozi wao ulirithi madeni kutoka uongozi uliopita hivyo wanaendelea kuyalipa madeni hayo

banner

“Tumerithi vitu vingi yakiwemo madeni kutoka kwa uongozi uliopita, hata hili deni ya Tambwe ni miongoni mwa madeni hayo. Tunawahakikishia Wanayanga kuwa deni hili litalipwa,” alisema Mwakalebela

Aidha Mwakalebela aliongeza kuwa pia watalipia fedha walizotakiwa walipe ili kesi yao dhidi Bernard Morrison iweze kusikilizwa na CAS

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.