Home Makala Mukwala Atwaa Tuzo Machi 2025

Mukwala Atwaa Tuzo Machi 2025

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya Simba sc Stephen Desse Mukwala amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya Nbc kwa mwezi machi akiwashinda Ellie Mpanzu na Pascal Msindo wa klabu ya Azam Fc ambao aliingia nao Fainali.

Kamati ya Tuzo iliyochini ya bodi ya ligi kuu ilimchagua Mukwala kutokana na kuonyesha kiwango kizuri akifunga mabao manne katika mwezi huo ikiwemo kufunga mabao matatu katika mchezo mmoja (Hattrick) dhidi ya Coastal Union jijini Arusha katika uwanja wa Sheikh amri Abeid Kaluta.

Mukwala ambaye alianza kwa kususua katika miezi ya mwanzo ya ligi kuu,siku za hivi karibuni amefanikiwa kukuza kiwango chake na kuwa na uhakika wan amba katika klabu hiyo na mara nyingine akimuweka benchi mshambuliaji Lionel Ateba.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited