Friday, May 9, 2025
Home Makala Kakolanya Atimuliwa Namungo Fc

Kakolanya Atimuliwa Namungo Fc

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa klabu ya Namungo Fc umemuondoa kikosini mwao golikipa  Beno Kakolanya kutokana na matukio ya utovu wa nidhamu ambayo amekuwa akiyafanya mara kwa mara.

Kakolanya ameondolewa kikosini humo alipokuwa akitumika kwa mkopo akitokea klabu ya Singida Black Stars na sasa atarejea katika klabu yake mkoani Singida.

banner

Kipa huyo mkongwe ambaye amezichezea klabu za Simba sc na Yanga sc kwa nyakati tofauti amekua na matatizo ya kinidhamu mara kwa mara tangu akiwa katika klabu hizo.

Mpaka sasa haijafahamika msimamo rasmi wa klabu yake ya Singida Black Stars kuhusu suala hilo kama itampokea ama lah.

Kakolanya katika ubora wake alikua ni kipa mwenye uwezo mkubwa hasa wa kucheza mipira ya uso kwa uso na washambuliaji hatari nchini kiasi cha kupata nafasi katika kikosi cha timu ya Taifa nchini.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.