Home Makala Ibrahim Class Amtwanga Mchina

Ibrahim Class Amtwanga Mchina

by Sports Leo
0 comments

Bondia Mtanzania Ibrahim Class ameshinda pambano la ubingwa wa TPBRC dhidi ya bondia raia wa China Xiao Tau Su katika pambano hilo la ubingwa wa Afrika lililofanyika katika ukumbi wa PTA sabasaba jijini Dar es salaam.

Pambano hilo ambalo ndio lilikua pambano kuu katika usiku huo ambapo katika mapambano ya utangulizi bondia Fadhil Majiha alifanikiwa kumpiga bondia kutoka Afrika ya kusini Bongani Mahlangu katika pambano la raundi 10 na kufanikiwa kupata mkanda wa ubingwa wa WBC (World Boxing Council).

Katika pambano hilo kuu Ibrahim Class ilimlazimu afanye kazi ya ziada kumthibiti Tau Su ambaye naye alikua moto kwa kupeleka ngumi za haraka haraka huku akitumia akili zaidi katika kujilinda.

banner

Uamuzi wa majaji baada ya raundi ya mwisho ndio uliompa ushindi Class kwa pointi huku akithibitisha ubora wa mpinzani wake huyo wakati wa mahojiano.

Mimi ni mwanaume na siyo mvulana”alisema Ibrahim Class wakati akiongea na waandishi ambapo alisema kuwa kama sio uimara na uzoefu wake basi angepoteza pambano hilo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited