Friday, May 9, 2025
Home Makala Carlinhos Awashukuru Mashabiki Yanga

Carlinhos Awashukuru Mashabiki Yanga

by Sports Leo
0 comments

Nyota mpya wa mabingwa wa kihistoria Tanzania bara, Yanga Sc “Carlos Stenio Guimaraes do Carmo” maarufu kama Carlinhos ametoa shukrani zake za dhati kwa mashabiki wote wa klabu hiyo kwa mapokezi makubwa ambayo yatabaki historia kwake.

Carlinhos aliwasili jana uwanja wa Mwl Julius Kambarage Nyerere saa saba mchana ambapo alikutana na umati mkubwa wa mashabiki wa Yanga tayari kumpokea na kumkaribisha nyumbani Jangwani.

Mashabiki hao walikuwa ni wengi sana kana kwamba waliikonga nafsi za nyota huyo na kujiona amefikia sehemu salama na kwa watu wenye ukarimu wa dhati kwani umoja wao ulishindwa kuzuilika hadi serikali ikaamua kuingilia ili kutuliza fujo zilizotokana na furaha.

banner

Carlinhos ambaye ni raia wa Angola amesema kuwa amefarijika sana kujiunga na Yanga Sc ambayo ni timu kubwa na tayari ameuona ukubwa wake kabla hajaingia uwanjani.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.