Home Soka Yanga sc Kurudi Kambini Leo

Yanga sc Kurudi Kambini Leo

by Sports Leo
0 comments

Mastaa wa kikosi cha Yanga sc wanatarajiwa kurudi kambini hii leo baada ya kupewa mapumziko ya siku mbili kwa ajili ya maombolezo ya msiba wa aliyekua Rais ya Jmt John Pombe Magufuri.

Mastaa hao walikua wanajifua kambini Avic Town kigamboni lakini waliruhusiwa siku ya Jumatatu na Jumanne kupumzika huku wakipata wasaa wa kumuaga Rais Magufuri aliyefariki machi 17.

Kurejea kwa mastaa hao kunamaanisha kuwa klabu hiyo itakua katika maandalizi kabambe ya kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Kmc huku pia wakitarajiwa kuwavaa Prisons katika mchezo wa kombe la Fa mkoani Sumbawanga.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited