Connect with us

Soka

11 wtu wanatosha kukipiga AFCON 2022

Shirikisho la soka Afrika(CAF) limetangaza kuwa kwenye mashindano ya kombe la mataifa Afrika mwaka huu timu itakayokuwa na idadi ya wachezaji 11 kwa kikosi kizima itaruhusiwa kucheza hata kama haina kipa rasmi ndani ya wachezaji hao.

Hayo yamejiri baada ya baadhi ya mataifa yaliyokwenda kushiriki mashindano hayo kuripoti maambukizo ya Uviko-19  mapema kabla ya mechi kuanza na kutishia uhai wa mashindano hayo makubwa barani Afrika.

CAF wamesema kuwa ili kukabiliana na changamoto hiyo na kutokuharibu ratiba ya mashindano hayo,Taifa litakolokuwa na maambukizi mengi ndani ya kikosi lakini walio wazima wanafika 11 basi mechi itapigwa kama ilivyopangwa bila kuahirishwa isipokuwa pale tu idadi ya ambao hawajaambukizwa ikiwa chini ya 11.

Wachezajim kadhaa kama beki wa Senegal Kalidou Kolibaly na Ismair Sarr wamekutwa na maambukizi ya uviko-19 ndani ya kikosi hicho.

Michuano hiyo itaanza rasmi hii leo kwa mchezo wa ufunguzi kati ya wenyeji Cameroon dhidi ya Burkina Faso majira ya saa moja usiku saa za Afrika Mashariki.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka