Home Soka Mbappe Kutua Genk

Mbappe Kutua Genk

by Sports Leo
0 comments

Imeripotiwa kuwa mshambuliaji kinda wa timu ya vijana ya Tanzania(Serengeti boys) Kelvin John “Mbappe” atajiunga na timu ya Krc Genk anayoichezea mtanzania Mbwana Samata ifikapo mwezi ocktoba mwaka huu.

Mbappe atajiunga na timu hiyo kama mwanafunzi anayesoma nchini humo ili kurahisisha taratibu za kucheza soka kwa kuwa ana umri mdogo na usajili kamili unatarajiwa kukamilika january mwakani wakati wa usajili wa dirisha dogo barani ulaya.

Kinda huyo licha ya kujiunga na timu hiyo tayari alishafanya majaribio na timu mbalimbali barani ulaya na Afrika hasa alipofanya majaribio nchini Denmark na Afrika kusini katika timu ya Ajax cape town ambao ni tawi la Ajax fc ya nchini Uholanzi majaribio ambayo alifuzu mbele ya kipa wa zamani wa Manchester united Edwin Van De Sar.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited