Wakati kikosi cha Simba sc kikiwa tayari hewani kuwafuata Us Gendamarie ya nchini Niger imebainika kwamba mastaa wanne wa kikosi cha kwanza wataikosa mchezo huo kutokana na matatizo mbalimbali yanayowakabili,
Kocha Pablo Franco amethibitisha kuwakosa Kibu Dennis na Hassan Dilunga pamoja na Chris Mugalu ambao wanasumbuliwa na majeraha huku kiungo Rally Bwallya yeye akiwa na ruhusu maalumu kufuatia kuwa na msiba nyumbani kwa nchini Zambia.
Simba sc inakwenda kuwavaa USGN ikiwa na alama tatu mkononi baada ya kuwafunga Asec Mimosa kwa goli tatu kwa moja mchezo uliofanyika hapa jijini Dar es salaam wiki iliyopita.