Timu ya Simba sc imemteua mtangazaji wa Bbc Salim Kikeke kuwa balozi wa timu hiyo katika jiji la London nchini Uingereza.
Taarifa iliyotolewa na bodi ya wadhamini ya klabu hiyo imeonyesha kuwa klabu hiyo imemteua mtangazaji huyo mwenye mapenzi na timu hiyo kuwa balozi katika jiji hilo maarufu duniani.
Kikeke ambaye anaishi nchini humo ataiwakilisha klabu hiyo katika mambo mbalimbali kama mshabiki na mwanachama ambapo moja ya kazi kubwa ni kuhakikisha timu hiyo inaongeza mashabiki jijini humo.