Connect with us

Soka

Hitimana Atimuliwa Namungo Fc

Klabu ya Namungo FC itakayoshiriki mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF Confederation Cup) imevunja mkataba na kocha wake Hitimana Thiery raia wa Burundi kwa makubaliano ya pande zote mbili na Kwa sasa timu hiyo itakuwa chini ya Kocha Hemedi Morocco kutoka Zanzibar.

Namungo ilifanikiwa kumaliza ligi kuu katika nafasi ya nne msimu uliopita huku ikifanikiwa kufika fainali ya michuano ya Azam Sports Confederation Cup ambako ilifungwa na Simba sc lakini ilibahatika kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa katika kombe la shirikisho baada ya Simba sc kutwaa taji la ligi na F.a hivyo kanuni kwapa nafasi Namungo Fc.

Kocha Hemed Morocco atakua na kibarua cha kuhakikisha timu hiyo inarejea katika ubora wake baada ya kumpoteza nyota wake Reliants Lusajo aliyejiunga na Kmc.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka