Home Soka CAF yaitoa Biashara United shirikisho

CAF yaitoa Biashara United shirikisho

by Sports Leo
0 comments

Shirikosho la mpira wa miguu barani Afrika (CAF) limeiondosha rasmi klabu ya soka ya Biashara United ya Mara katika michuano ya kombe la shirikisho baada ya kushindwa kucheza mchezo wa marudiano dhidi ya Al Ahly Tripoli.

Biashara ilishindwa kusafiri kucheza mchezo huo uliopaswa kufanyika Novemba 23 nchini Libya kutokana na kile walichodai kukosa vibali vya kutua katika anga za nchi za Sudan na Ethipoia.

Katika mchezo wa awali ulifanyika kwa Mkapa Biashara ilipata ushindi wa magoli 2-0 na kuweka matumaini ya kufuzu mbele.

banner

Taarifa rasmi ya CAF imetolewa na shirikisho la soka nchini(TFF) na kusema kuwa sababu iliyotolewa na Biashara haijitoshelezi kuwafanya kucheza mchezo wa marudiano kwa kusogezwa mbele mchezo huo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited