Connect with us

Soka

Aussems Bado Utata Simba

Ofisa Mtendaji wa klabu ya Simba, Senzo Mazingisa, amesema Kocha Mbelgiji, Patrick Aussems alimtumia ujumbe ukimwarifu kuwa amepatwa na dharura.
Taarifa imesema kuwa Aussems alimtumia Mazingisa ujumbe huo lakini hakuanisha kuwa ameelekea wapi japo inalezwa alisafiri kuelekea kwao Ubelgiji.
Mazingisa amesema Aussems hakumwambia kuwa anaelekea wapi na ameahidi kulitolea ufafanuzi zaidi pale atakaporejea nchini.
“Aussems bado ni mwajiriwa katika klabu ya Simba.
“Alinitumia ujumbe Jumatatu kuwa ana dharura lakini hakueleza kuwa anaelekea wapi, akisharejea nitakuwa na ya kueleza,” amesema Mazingisa.
Cc:SaleheJembe

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka