Mwanariadha Mtanzania Alphonce Simbu amefanikiwa  kushika nafasi ya pili katika Shanghai Marathon 2023 na huku Mtanzania mwingine Jackline Sakilu ambaye ameshika nafasi ya nane katika mashindano hayo maarufu nchini humo.
Pamoja na kupata medali katika mashindano hayo wanariadha hao wamefanikiwa kufuzu kushiriki Mashindano ya Olympic 2024 na Wataungana na Wanariadha wengine watanzania Gabriel Gerald Geay na Magdalena Chripine ambao tayari walishafuzu kushiriki Olympic 2024.
Shanghai Marathon ambazo hufanyika nchini china ni moja ya marathon zenye thamani kubwa nchini humo ambazo hufanyika barabarani katika mitaa mbalimbali jijini humo ambapo washiriki zaidi ya elfu moja walishindana katika mbio za kilometa 42.5.