Connect with us

Masumbwi

Tyson Fury kustaafu tena Boxing

Bondia wa uzito wa juu duniani toka Uingereza Tyson Fury ametangaza kuwa atastaafu ngumi za kulipwa baada ya mapambano yake matano ya mwisho ndani ya miaka miwili.

Bingwa huyo anayeshikilia ubingwa wa WBC baada ya kumpiga Mmarekani Deontay Wilder mwaka 2020 ameeleza pia kuwa anatarajia kuingia kwenye ukufunzi wa mchezo huo wa ngumi mara baada ya kutundika gloves zake.

Fury ameyataja mapambano hayo ni mawili dhidi ya Muingereza mwenzake Anthony Joshua,pambano la tatu dhidi ya Deontay Wilder,lingine ni dhidi ya Dillian Whyte na la mwisho ni dhidi ya bondia mwenye maneno mengi Derek Chisora.Wilder amejipanga kubakia katika mchezo huo na kuwapa mafuzo mabondia chipukizi.

Tyson alisema kuwa ”Nitakampomaliza kama bingwa labda baada ya mapambano matano hivi,nitapumzika,nitaingia kutengeneza vijana na tunaamini tutapata bingwa mpya wa dunia pengine bora zaidi kuliko mimi”.Kwangu ni maamuzi magumu sababu najua ni nini ambacho naweza bado kufanya nikiwa ulingoni”.Hivyo itakuwa ni changamoto haswa”.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Masumbwi

  • Mwakinyo Huru

    Kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini (TPBRC) imemfungulia bondia Hassan Mwakinyo kutoka kifungoni baada...

  • Bondia Mtanzania Fadhili Majiha ‘Kiepe Nyani’ ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC Afrika...

  • Ibrahim Class Amtwanga Mchina

    Bondia Mtanzania Ibrahim Class ameshinda pambano la ubingwa wa TPBRC dhidi ya bondia raia...

  • Mwakinyo Aitwa Mahakamani

    Kampuni ya PAF Promotion imemfungulia shauri la madai Bondia Hassan Mwakinyo ambalo linatarajiwa kutajwa...