Home Makala Yanga sc Yaambulia Alama Moja Kwa Jkt

Yanga sc Yaambulia Alama Moja Kwa Jkt

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imeshindwa kuchukua alama tatu katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc nchini dhidi ya Klabu ya Jkt Tanzania uliofanyika katika uwanja wa Mbweni jijini Dar es Salaam.

Ikitoka kushinda takribani michezo sita mfululizo ya ligi kuu kwa idadi kubwa ya mabao,pia ilitarajiwa kupata ushindi katika mchezo huo uliokua ukisubiriwa kwa hamu.

banner

Ikianza na kikosi chake cha kila siku kikiwa na mastaa Clement Mzize na Cletous Chama sambamba na Prince Dube ambao waliongoza mashambulizi hayo wakisaidiwa na Pacome Zouzoua sambamba Mudathir Yahaya ambao kipindi cha kwanza walikosa nafasi kadhaa za mabao.

Uimara wa safu ya ulinzi ya Jkt Tanzania ulizidi kupoteza matumaini kwa Yanga sc kuibuka na ushindi katika mchezo huo huku licha ya mwalimu Hamdi Miloud kufanya mabadiliko ya kuwaingiza Maxi Nzengeli,Stephen Aziz Ki na Kennedy Musonda bado hali ilikua mbaya kwa Yanga sc.

Dakika tisini za mwamuzi Ahmed Arajiga kutoka mkoani Manyara zilikamilika kwa Yanga sc kupata alama moja ambayo imewafanya kukaa kileleni wakiwa na alama 46 wakicheza michezo 18 ya ligi kuu huku Jkt Tanzania wakiwa nafasi ya tisa ya msimamo wakiwa na alama 20 katika michezo 18 ya ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited