Home Makala Yanga Sc Njia Nyeupe kwa Gilbertinho

Yanga Sc Njia Nyeupe kwa Gilbertinho

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Petro de Luanda imepanga kusitisha mkataba wa winga , Deivi Gilberto, aliyejiunga na klabu hiyo kwa mkopo kutoka Orlando Pirates kutokana na mchezaji huyo kuwa utovu wa nidhamu klabuni hapo na kushindwa kuitumikia Petro de Luanda kwa usahihi.

Taarifa zinaripoti kuwa winga huyo amekuwa na tabia mbaya nje ya uwanja jambo ambalo Klabu hiyo imechoshwa na tabia hiyo. Aidha awali kulikuwa na taarifa za chini Kuwa klabu kutoka Tanzania zinahitaji saini yake lakini bado hakuna klabu iliyoweka wazi kama inahitaji saini ya winga huyo.

Yanga sc ni miongoni mwa klabu ambayo ilikuwa inatajwa kuhitaji saini ya winga huyo , mpaka wakati hii tayari Yanga wameshamalizana na Mshambuliaji wao Musonda ambae hatakuwa sehemu ya Kikosi hicho msimu ujao hivyo taarifa zinaripoti kuwa nafasi yake atachukua winga huyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited