Uongozi wa timu ya KMC imefikia makubaliano ya kusitisha mikataba ya wachezaji watano na wa sita kumuuza mkoani Mtwara katika timu ya Ndanda Fc.
Wachezaji Aaron Lulambo,George Sangija,Rehani Kibingu,Melly Mongolare, na Janvier Besala Bokongu wamesitishiwa mkataba ikiwa sababu kubwa ni kushindwa kuonyesha uwezo wao uwanjani.
Vitalisi Mayanga ameuzwa kwa timu aliyoichezea zamani Ndanda Fc kabla ya kusajiliwa kwa kandarasi ya miaka miwili KMC.