Home Makala Simba Sc Yashindwa Kufurukuta kwa Al Hilal Fc

Simba Sc Yashindwa Kufurukuta kwa Al Hilal Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba Sc imeambulia sare ya 1-1 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Klabu ya Al Hilal Fc uliofanyika katika uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Simba sc ilitangulia kupata bao la kwanza dakika ya 26 ya mchezo likifungwa na Lionel Ateba baada ya shambulizi zuri lililoanzishwa na Ladack Chasambi.

banner

Simba sc ilitawala mchezo huo huku ikionyesha kuanza kuelewana hasa eneo la kiungo na mabeki ambapo kocha Fadlu Davis ana kazi ya kutengeneza maelewano eneo la ushambuliaji.

Kocha Florent Ibenge aliwaongoza vyema mastaa wa Al Hilal Fc ambao waliwakosa baadhi ya mastaa waliokwenda kujiunga na timu zao za Taifa na kufanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 86 ya mchezo.

Mpaka dakika 90 za mchezo huo zinamalizika matokeo yalibaki 1-1 huku baadhi ya mashabiki wa Simba sc wakionyesha kuridhika na kiwango cha timu na mastaa mmoja mmoja akiwemo Deborah Fernández.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited