Connect with us

Makala

Simba sc Yalamba Udhamini M-bet

Klabu ya Simba sc imefanikiwa kuingia mkataba wa udhamini wa jezi na kampuni ya michezo ya kubashiri ya M-bet mkataba ambao unasidikika kuwa ni mnono kwa muda wa miaka mitano ambapo kampuni hiyo italipa kiasi cha Shilingi za kitanzania Bilioni Tatu kila mwaka.

Japokua Simba sc haijatangaza rasmi dili kuhusu dili hilo tayari hivi leo mastaa wa timi hiyo wameonekana wakiwa wamevalia jezi zenye nembo ya kampuni hiyo wakati wakiwa uwanja wa ndege wa Julias Nyerere wakielekea nchini Misri kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya msimu mpya.

Habari za ndani zinadai kuwa klabu hiyo imeingia mkataba na kampuni hiyo wa miaka mitano wenye thamani ya bilioni 15 za Kitanzania huku pia kukiwa na kipengele cha kufanya mapitio ya mkataba kila msimu.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala