Home Makala Simba sc Vs Ihefu Fc Shirikisho

Simba sc Vs Ihefu Fc Shirikisho

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc itavaana na Ihefu Fc katika mchezo wa kombe la shirikisho nchini kwa mujibu wa droo iliyofanyika mapema hivi leo katika ofisi za wadhamini wa michuano hiyo za Azamtv jijini Dar es salaam.

Kwa mujibu wa Droo hiyo iliyoongozwa na Said Maulid staa wa zamani wa Yanga sc na Bonifasi Pawasa staa wa zamani wa Simba sc imeonyesha kuwa Simba sc itaanzia nyumbani huku endapo moja kati ya klabu hizo zitafuzu basi zitavaana na mshindi kati ya Azam Fc na Mtibwa Sugar.

Mwaka jana katika michuano hii Simba sc iliishia katika hatua ya nusu fainali ambapo ilifungwa na Yanga sc bao 1-0 huku Yanga sc ikifanikiwa kuchukua kombe hilo baada ya kuifunga Coastal Union katika mchezo wa fainali jijini Arusha.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited