Home Soka Simba Queen Watawala Tuzo TFF

Simba Queen Watawala Tuzo TFF

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Simba Queen imefanikiwa kutawala usiku wa Tuzo za Shirikisho la soka nchini baada ya kufanikiwa kutwaa takribani tuzo nyingi za soka la wanawake nchini katika usiku wa Tukio hilo lililofanyika katika ukumbi wa Super Dome Masaka Jijini Dar es salaam.

Simba queen ilikua na washiriki kutoka vipengele vya kocha bora,kipa bora,mfungaji bora na mchezaji bora ambapo ilifanikiwa kunyanya tuzo ya Mchezaji bora iliyochukuliwa na Aisha Mnuka ambaye pia alichukua tuzo ya mchezaji bora na Juma Mgunda alichukua tuzo ya kocha bora.

Kwa upande wa kipa bora wa ligi kuu ya Wanawake ilikwenda kwa Caroline Rufaa wa Simba Queen na kuifanya timu hiyo kukosa tuzo moja pekee katika ya tuzo sita ambazo iliingiza washiriki katika tukio hilo.

banner

Msimu huu Simba Queen chini ya kocha Juma Mgunda imefanikiwa kutwaa taji la ligi kuu ya soka ya wanawake nchini na inatarajiwa kuingia katika michuano ya kanda ili kuwania nafasi ya kuingia katika michuano ya mabingwa barani Afrika.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited