Beki mkongwe wa Tanzania Erasto Edward Nyoni ambaye alikua na majeraha yaliyomfanya kukosa mchezo wa ufunguzi wa fainali za mataifa ya Afrika(Afcon) dhidi ya Senegali imeripotiwa amepona majeraha hayo na tayari ameshaanza mazoezi kamili na kikosi cha timu ya taifa kilichopo nchini Misri.
Erasto aliumia katika mechi ya kujiandaa na michuano hiyo dhidi ya Zimbabwe iliyoisha kwa timu hiyo kutoka sare huku pia Tanzania ilimpoteza beki mwingine Aggrey Morris ambaye ametolewa katika kikosi baada kugundulika majeraha yake yatachukua muda mrefu kupona na nafasi yake kuzibwa na David Mwantika.
Tanzania imepoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Senegali baada ya kukubali kipigo cha mabao mawili kwa bila na kesho Alhamisi wataivaa kenya katika mchezo wa pili utakaopigwa saa tano usiku.