Home Makala Mukoko Kupaa Congo

Mukoko Kupaa Congo

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa Yanga anatarajia kuondoka leo jioni kuelekea DR Congo kujiunga na kikosi cha timu ya Taifa ya nchini humo, kujiandaa na michezo za kufuzu AFCON.

Mukoko ni miongoni mwa nyota 30 walioitwa katika kikosi hicho kinachojiandaa na michezo hiyo kutafuta tiketi ya kufuzu Afcon ambapo michuano iliyopita nchini Misri Congo ilitolewa mapema.

Ofisa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Hassan Bumbuli, amethibitisha kuwa mchezaji huyo muda wowote atajiunga na kambi ya kikosi cha Congo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited