Connect with us

Makala

Msuva Atua Uarabuni

Aliyekua mshambuliaji wa klabu ya Wydad Casablanca Simon Msuva amejiunga na klabu ya Alqadsiah inayoshiriki ligi daraja la pili nchini  Saudi Arabia ambapo amesaini mkataba wa mwaka mmoja wenye kipengele cha kuongeza mwingine zaidi.

Winga huyo hakua na timu kwa muda mrefu kutokana na kuwa na mgogoro kuhusu fedha za usajili na mishahara na klabu hiyo ya Wydad ambayo ilimsajili kutoka Difaa El Jadid ya huko huko nchini Morroco kiasi cha kesi kufika katika Shirikisho la soka Duniani (Fifa) ambao waliamuru klabu hiyo kumlipa mchezaji huyo kiasi cha Bilioni 1.6 ikiwemo pamoja na fidia.

Usajili huo unahitimisha tetesi za awali kuwa anaweza kusalia nchini Tanzania kujiunga na klabu yake ya zamani ya Yanga sc huku pia alikua akihusishwa kujiunga na Simba sc.

Msuva atajumuika na mchezaji wa zamani wa Nkana Fc ya Zambia na Al ahly Sc Walter Bwallya katika klabu hiyo inayoshiriki ligi daraja la pili nchini humu huku ikisemekana atalipwa kiasi kikubwa cha mshahara kwa wiki.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala