Klabu ya Afc Arusha imetangaza kifo cha Kocha Msaidizi wa klabu hiyo Luke Juma kilichotokea hapo Jana.
Habari iliyotolewa leo kwenye vyombo vya habari na ofisa habari wa klabu hiyo, Bahati Msilu imeeleza kuwa Luke amefundisha Afc Arusha kwa nyakati tofauti akiwa ni kocha mpaka umauti unamkuta akiwa kama kocha Msaidizi wa klabu hiyo akishirikiana na Mwalimu Ulimboka Mwakingwe.
Afc Arusha wanatoa pole kwa familia ya Marehemu, ndugu jamaa,marafiki wote na Familia ya wapenda michezo wote hapa nchini.