Serikali la Brazili imepinga vikali kitendo cha klabu ya Flamengo kuruhusu wachezaji wake kurejea mazoezini ili hali serikali bado haijaruhusu.
Flamengo ambao walishinda taji la ligi na Copa Libertadores mwaka 2019 iliwaita wachezaji wake kurejea na kuanza mazoezi siku ya Jumatatu hii ni baada ya miezi 2 ya ligi Nchini humo kusimamishwa kutokana na janga la Covid-19 lililoikumba Dunia.