Home Makala Feisal,Mzize Wang’ara Crdb Cup

Feisal,Mzize Wang’ara Crdb Cup

by Sports Leo
0 comments

Kiungo mshmabuliaji wa klabu ya Azam Fc Feisal Salum  amefanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa kombe la Shirikisho huku Clement Mzize na Djigui Diarra wa klabu ya Yanga sc wakitwaa tuzo za mfungaji bora na kipa bora katika usiku wa tuzo hizo zilizotolewa na Shirikisho la soka nchini (TFF) katika ukumbi wa The Super Dome Masaki Jijini Dar es salaam.

Feisal katika tuzo hizo akimzidi Stephane Aziz Ki wa Yanga sc na kipa Djigui Diarra ambaye wengi walitarajia kuwa anaweza kupata kutokana na kuonyesha uwezo wa juu katika michuano hiyo.

Mzize yeye alifanikiwa kupata tuzo ya mfungaji bora wa michuano hiyo baada ya kulingana mabao na Edward Songo wa Jkt Tanzania lakini alifaidika na kipengele hicho kutokana na mabao yake kuifikisha timu hiyo fainali na kunyanyua taji hilo.

banner

Diara yeye aliwazidi Aboubakar Khomeiny na Mohamed Mustapha wa Azam Fc na kufanikiwa kutwaa tuzo hiyo ambayo wengi waliitarajia kutokana na mafanikio ya kipa huyo kwa siku za karibuni akiisaidia Yanga sc kutwaa taji la ligi kuu na michuano ya kimataifa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited