Home Soka Fadlu,Ahoua Walamba Tuzo za August

Fadlu,Ahoua Walamba Tuzo za August

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa Klabu ya Simba Sc Fadlu Davis sambamba na kiungo mshambuliaji wa klabu hiyo Jean Charles Ahoua wameibuka kuwa Kocha bora na mchezaji bora wa ligi kuu ya Nbc nchini kwa mwezi huu wa nane.

Waajiriwa hao wa klabu ya Simba Sc wamelamba tuzo hizo mapema hivi leo ambapo wametangazwa na bodi ya ligi kuu nchini ambayo hufanya tathmini kuhusu nani anafaa kuchukua tuzo hizo.

Tplb katika taarifa yake kwa umma imetangaza kuwa Fadlu amepata nafasi hiyo baada ya kuwezesha Simba sc kuchukua alama sita na mabao saba ambapo ilifanikiwa kushinda michezo miwili mfululizo ya ligi kuu dhidi ya Tabora United na Fountain Gate Fc.

banner

Ahoua yeye alifanikiwa kufunga bao moja huku akitoa usaidizi wa upatikanaji wa mabao matatu katika michezo hiyo miwili ya ligi kuu ya Nbc.

Mpaka sasa ambapo ligi Imesimama Simba sc imejikita kileleni mwa msimamo ikiwa na alama sita na mabao saba katika michezo miwili ya ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited