Home Makala Azam Fc Yakomaa na Ibenge

Azam Fc Yakomaa na Ibenge

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imeanza mazungumzo na kocha wa klabu ya Al Hilal Fc Florent Ibenge ili kuinoa klabu hiyo kuchukua nafasi ya kocha Yousouph Dabo iliyemtimua wiki iliyopita.

Azam Fc inaamini Ibenge ni mtu sahihi kuchukua nafasi ya Dabo kutokana na kuwa na wasifu mzito akizifundisha klabu za As Vita,Rs Berkane na kufanikiwa kuzipatia mataji kadhaa makubwa barani Afrika.

Ibenge ambaye kwa sasa anaifundisha Al Hilal Fc ni kocha wa gharama kummliki ambapo mabosi wa Azam Fc wameamua kutojali kuhusu fedha wakitazama mafanikio zaidi kutokana na kuwa na mastaa wa gharama kikosini humo.

banner

Azam Fc pia iliwahi kumtaka Nasredine Mohammed Nabi aliyekua kocha wa zamani wa Yanga sc lakini kocha huyo hakua tayari kuachana na klabu yake ya Kaizer Chiefs Fc ya nchini Afrika ya Kusini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited