Home Makala Simba sc Waifuata Dynamos

Simba sc Waifuata Dynamos

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha Simba sc kimeondoka mchana huu kuelekea Ndola Zambia tayari kwa mchezo wa raundi ya kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Power Dynamos utakaochezwa Jumamosi hii uwanja wa Levy Mwanawasa.

Kikosi hicho kilichoonekana uwanja wa ndege wa mwalimu J.K Nyerere jijini Dar es salaam kimejaa mastaa wa klabu hiyo akiwemo kipa mpya Ayoub Lakred pamoja na mastaa kama Che Fondoh Malone,Leandre Onana,Cletous Chama,Luis Miqquisone,Moses Phiri,Jean Baleke,Mzamiru Yassin na mastaa wengine kama inavyoonekana hapa.

banner

Simba sc watakua na kazi ya kuhakikisha wanapata matokeo mazuri ugenini ili waje kuimaliza kazi vizuri nyumbani na kufanikiwa kufuzu hatua ya makundi ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika ambapo msimu uliopita walitolewa na Wydad Casablanca hatua ya robo fainali.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited